Baada ya mazungumzo marefu ya usiku
mjini Brussels, mawaziri hao pia wamekubaliana kuingiza utaratibu wa
kusamehe madeni katika kipindi cha miaka miwili -- sharti kubwa kwa
Athen na shirika la Fedha Duniani.
Jopo hilo la mawaziri kumi na
tisa limesema makubaliano hayo yamewezekana kuwa rahisi kutokana na
jitihada za Ugiriki za kufanya mabadiliko ya kiuchumi.Mkuu wa viongozi hao wa Jumuia ya Ulaya, Jeroen Dijselbloem ameitaja hatua hiyo kuwa ni kubwa zaidi.
IMF imeipokea kwa mikono miwili hatua hiyo ya kutambua kuwa hali ya mdororo wa kiuchumi imepitiliza hivyo utaratibu wa kusamehe madeni unahitajika.
0 comments:
Post a Comment