Maonyesho
ya bidhaa z Plastiki yaliyoanza jana Mei 27.2016 katika ukumbi wa
Mlimani City, Jijini Dar es Salaam yanatarajia kufikia tamati hiyo kesho
Jumapili ya Mei 29.
Maonyesho
hayo ambayo Tanzania ni mwenyeji kwanza ya bidhaa za plastiki,
mpira, kemikali za petrol na ujenzi yanakuwa ya kipekee huku watu
mbalimbali wameendelea kujitokeza kwa wingi katika ukumbi wa Kituo cha
Mikutano cha Mlimani City jijiniDare s Salaam.
Awali
Meneja Mkuu wa Expo One, Ahmed Barakat ambao ni waandaaji wa maonyesho
hayo, alisema nchi zote za Afrika Mashariki na kati zinashiriki katika
maonesho hayo.
Afrika
–PPB-EXPRO ni jukwaa la kipekee la bidhaa mpya na yatatoa mwanya wa
kuyaelewa masoko yake ambayo hayafahamiki vizuri.
“Maonesho
haya yamebuniwa kwa lengo la kukuza umoja miongoni mwa Waafrika kwa
kuimarisha mahusiano ya kibiashara kati ya Misri na Tanzania na hali
kadhalika kuyaweka masoko yake kwenye ramani ya Afrika,kubainisha kuwa
Tanzania ni ya kwanza katika orodha ya nchi za Afrika ambapo
Africa-PBB-EXPO imepanga kushirikiana nayo.
Alisema
kupitia Aramex na kwa uratibu wa TanTrade na Taasisi ya Sekta Binafsi
Tanzania (TPSF), Africa-PBB-EXPO inatoa fursa ya kipekee kwa
waoneshaji walio na kanzidata za kina kusajiliwa mara zinapopokelewa.
Barakat
alitoa wito kwa wafanyabiashara kushiriki katika maonesho hayo ili
kuweza ‘kubaini fursa za ushirikiano katika masoko haya mapya pamoja na
mtandao ulio na wateja na wenza wa kibiashara.
0 comments:
Post a Comment