VIGOGO wa Germany Bayern Munich leo Usiku wanatinga Uwanjani kwao Allianza Arena kurudiana na Atletico Madrid ya Spain katika Mechi ya Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI huku wakitakiwa kupindua kipigo cha Bao 1-0 ili wao watinge Fainali.
Wiki iliyopita huko Vicente Calderon Jijini Madrid na Bao la Dakika ya 11 la Niguez liliwapa Atletico ushindi wa 1-0.
Bayern wanatinga kwenye Mechi hii muhimu wakiwa na Majeruhi kadhaa ambao ni Holger Badstuber, Arjen Robben na Franck Ribery ambae huenda akarejea.
Atletico wao hawana Wachezaji majeruhi.
VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:
Bayern Munich: Neuer; Lahm, Boateng, Martinez, Alaba; Muller, Vidal, Thiago; Costa, Lewandowski, Ribery
Atletico Madrid: Oblak; Juanfran, Godin, Gimenez, Luis; Saul, Gabi, Fernandez, Koke; F Torres, Griezmann
REFA: Cüneyt Çakır (Turkey)
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment