Kiungo wa Tottenham Hotspur, Mousa Dembele amepewa adhabu ya kutokucheza michezo sita na Chama cha Soka Uingereza kwa kumkwaruza katika jicho mshambuliaji wa Chelsea, Diego Costa wakati timu hizo zilipombana Jumatatu iliyopita.
Kocha wa Tottenham, Mauricio Pochettino amethibitisha Dembele kupewa adhabu hiyo ambayo itamfanya kukosa michezo iliyosalia ya msimu huu na mingine ya msimu ujao utakaoanza mwezi Agosti.
Tottenham imebakiza michezo miwili hivyo Dembele ataukosa mchezo wa Southampton na Newcastle United na michezo mingine minne itakuwa ya msimu wa 2016/2017.
0 comments:
Post a Comment