Comments


ZAWADI NONO KWA MWALIMU ATAKAE FAULISHA MWANAFUNZI KATIKA SOMO LAKE

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameahidi kutoa zawadi ya fedha kwa mwalimu atakayefaulisha mwanafunzi katika somo lake la sayansi, lengo likiwa ni kutoa motisha kwa walimu.

Makonda aliyasema hayo  wakati akizindua programu ya kuwasaidia wanafunzi waliotoka katika familia masikini iliyoandaliwa na shule za Feza.12-Makondaa
Feza wametoa Sh milioni 37.5 kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi 150 wanaotoka katika familia masikini.

Makonda alisema atatoa Sh milioni 15 kwa mwalimu wa sekondari atakayefaulisha mwanafunzi katika masomo ya Sayansi na Sh milioni 10 kwa mwalimu wa kidato cha pili atakayefaulisha mwanafunzi katika masomo ya sayansi na Sh milioni tano kwa mwalimu wa shule ya msingi atakayefaulisha mwanafunzi.

“Niseme sitaishia kwenye kutoa fedha pekee, mwalimu huyo na familia yake watachagua mbuga yoyote ya wanyama watakayoitaka na nitagharamia kila kitu, naamini kwa kufanya hivyo kutajenga motisha hata kwa walimu wengine kuongeza jitihada na kuhakikisha anafaulisha wanafunzi,” alisema Makonda.

Aidha, Makonda amewashukuru Feza kwa kuamua kuwasaidia wanafunzi hao na amewataka wazazi kuhakikisha wanasimamia vyema fedha hizo ili zifanye kazi iliyokusuduwa.

“Sitopenda kusikia mama ametumia fedha hizo tofauti na nyinyi wanafunzi muwalipe wafadhili hawa kwa kusoma kwa bidii, hakuna mtu atakubali kuendelea kutoa msaada kwa mtu ambaye haoneshi juhudi,” aliongeza Makonda.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Shule hizo, Isa Otcu alisema shule hizo zimeamua kutoa msaada huo kwa ajili ya kumuunga mkono Rais John Magufuli katika harakati zake za elimu bure.

Alisema programu hiyo itatoa kiasi cha Sh 250,000 kwa kila mwanafunzi na tayari wameshaweka kiasi cha Sh 100,000 katika akaunti za wanafunzi hao kuanzia Januari mpaka Aprili.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments System

Disqus Shortname

Comments system