Comments


CHRIS BROWN AKIRI KUTAKA KUJIUA KISA RIHANA


Chris Brown amesema alitaka kujiua baada ya kumshambulia aliyekuwa mpenziwe Rihanna kabla ya tuzo za Grammy mwaka 2009.

Katika kipande kifupi cha makala yake ya ‘Karibu katika maisha yangu’,mwanamuziki huyo wa mtindo wa R & B amesema uhusiano wao ulikuwa kama ndoto lakini akajihisi kama hayawani.

“Nilikuwa katika kilele cha dunia,nyimbo zangu zikiongoza,nikapendwa na wengi nchini Marekani kabla ya kuanguka hadi kuwa adui wa umma,” alisema Chris Brown.

Kesi yake ilisitishwa mwaka jana baada ya jaji mmoja kusema kuwa nyota huyo amekamilisha mahitaji yake yote na kufunga kesi hiyo rasmi.

Pia kwenye makala hiyo inayowaonyesha Jennifer Lopez,Usher,Mike Tyson,Jamie Fox na Rita Ora, Chris Brown anasema, “Nilihisi kama nyota, lakini nilijiharibia. Nilikuwa nikilala.Sikuweza kula,nilijihisi maarufu,” alikiri.

Source: BBC
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments System

Disqus Shortname

Comments system