Comments


ZAIDI YA WAKAZI 500 WAVAMIA SHAMBA LA MWEKEZAJI ARUMERU


aru
Mgogoro mkubwa umeibuka katika kijiji cha Kwa Ugolo wilayani Arumeru mkoani Arusha baada ya zaidi ya wakazi 500 wa kijiji hicho kuvamia shamba la mwekezaji na kwa madai shamba hilo ni mali yao halali.
 
Tukio hilo lilitokea juzi wilayani humo ambapo wananchi hao walivamia shamba la kampuni ya Flycathter lenye ukubwa wa ekari 106  na kisha kuanza kujigawia ardhi huku wakisisitiza kwamba hawana mahali pa kwenda kulima.
 
Akizungumza katika eneo la tukio mkazi wa eneo hilo,Eliakim Mollel alisema ya kwamba shamba hilo ni halali yao kwa kuwa wamekuwa wakifanya shughuli nbalimbali kama kulima na kuokota kuni kabla ya wawekezaji hao kulichukua.
 
Mollel,alisema kwamba kumekuwa na mvutano mkubwa baina yao na wawekezaji hao kugombea shamba hilo kwa kipindi kirefu jambo ambalo limepelekea mahusiano mabovu baina ya pande mbili.
 
Baadhi ya wakazi wengine wa eneo hilo kwa nyakati tofauti bila kutaja majina yao hadharani walisema kwamba wameamua kuvamia na kugawana ardhi ndani ya shamba hilo kwa kuwa wamekosa sehemu ya kulima na kukosa hata mlo mmoja kwa siku.
 
Wakazi hao walidai kwamba wamevumilia kwa muda mrefu lakini serikali haitaki kuwakabidhi haki yao na kusisitiza kwamba wamechoka kuvumilia na kuamua kuchukua hatua ya kuvamia na kisha kugawana shamba hilo ili wafanye shughuli mbalimbali.
 
Akizungumzia tukio hilo meneja wa shamba hilo aliyejitambulisha kwa jina la Aikbar alisema kuwa shamba hilo ni mali yao kisheria na wanashangazwa na hatua ya wakazi hao kuvamia na kisha kujigawia maeneo.
 
Alisema kwamba tayari wameshatoa taarifa mbele ya jeshi la polisi huku akisisitiza kwamba wamepata hasara ya kiasi cha zaidi ya sh,500 milioni baada ya wananchi kuvamia na kisha kukata mazao pamoja na kuharibu mali mbalimbali zilizopo ndani ya shamba hilo.
 
Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Arusha,Charles Mkumbo ameliambia gazeti hili kwamba jeshi lake lina taarifa kuhusu tukio hilo na linaendelea kusimamia usalama wote na kuwataka wananchi wa eneo hilo kufuata sheria,kanuni  na taratibu endapo wakitaka kudai haki yao bila kuleta uvunjifu wa amani
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments System

Disqus Shortname

Comments system