Comments


AL AHLY YATUA DAR KWAAJILI YA KUMENYANA NA YANGA



Uongozi wa klabu ya Dar Es Salaam Young Africans leo April 6 kupitia kwa afisa habari wake 

Jerry Muro ameongea na vyombo vya habari na kuelezea taarifa za mchezo wao wa klabu 

Bingwa barani Afrika dhidi ya Al Ahly ya Misri utakaochezwa April  9 2016 uwanja wa Taifa Dar 

Es Salaam.

Jerry amethibitisha  Al Ahly kuwasili Dar Es Salaam alfajiri ya leo, pamoja na CAF kutoa majina 

ya waamuzi wa mchezo huo ambao wanatoka Ivory Coast Denis Dembele, Mauris Donatien, 

Moussa Bayere, Tangba Kambou lakini kamisaa wa mchezo Celestine Ntangungira anatokea 

Rwanda.



Hadi sasa Yanga mechi zao zilizopita za klabu Bingwa Afrika waligoma zisioneshwe kwenye TV ” 

Kwa sasa viongozi wanafanya utaratibu wa kuangalia namna ambavyo tunaweza kuruhusu TV 

kuonesha mchezo huo, lakini watu wajue tutaruhusu matangazo ya TV yarushwe mikoani kasoro 

Dar na Pwani ndio maana tumeweka kiingilio cha chini elfu tano” >>> Jerry Muro
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments System

Disqus Shortname

Comments system