Comments


UNENE WA MPONZA NASRI

 Kiungo wa  kati wa Manchester City Samir Nasri amepigwa marufuku kushiriki mazoezi ya pamoja baada ya kuongeza uzani kupindukia.
Kocha Pep Guardiola amethibitisha kuwa sababu yake kumuacha nje kiungo huyo ni kunenepa.
Nasri, 29, aliachwa nje hata baada ya wachezaji wote wa akiba kutumika katika mechi dhidi ya Borussia Dortmund nchini China.
Hapo jana mlinzi Gael Clichy alitambua sababu ya kukosekana kwa baadhi ya wachezaji katika kambi ya mazoezi kuwa ni kunenepa.

Meneja huyo mpya wa Manchester City Pep Guardiola amewapiga marufuku wachezaji waliozidi uzito, kufanya mazoezi na kikosi cha kwanza.
Pep amesema uzito ni jambo muhimu na kuwa wachezaji lazima waepuke baadhi ya vyakula na vinywaji.

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments System

Disqus Shortname

Comments system