Comments


WANAWAKE UGANDA WAAMUA KUANDAMANA


Image captionWanawake waandamana nchini Uganda
Kundi la wanawake nchini Uganda wanaopinga kuvuliwa nguo kwa mwenzao wakati alipokuwa akikamatwa na maafisa wa polisi, limefanya maandamano na kujaribu kuelekea bungeni ili kuwasilisha hoja yao dhidi ya ukatili wa maafisa wa polisi.
Hatua hiyo inajiri baada ya mwanamke mmoja kutoka chama cha Upinzani cha Forum for Democratic Change kinachoongozwa na Kizza Besigye kuvuliwa nguo na maafisa wa polisi alipokuwa akikamatwa wikendi iliopita.
Image captionWaandamana Uganda
Hatahivyo waandamanaji hao walizuiliwa kuendeleza maandamano hayo na kusukumwa hadi katika afisi zao na maafisa wa polisi.
Kulikuwa na jaribio la kuwakamata baadhi yao lakini walikataa.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments System

Disqus Shortname

Comments system