Comments


JK Azindua Mtambo Wa Umeme Kinyerezi





Rais wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi mtambo wa kufua umeme kutokana na Gesi Asilia huko Kinyerezi jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwakilishi wa Benki ya African Development (ADB) Bi. Tonia Kandiero na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO Felchesmi Mramba.
Rais wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi mtambo wa kufua umeme kutokana na Gesi Asilia huko Kinyerezi jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwakilishi wa Benki ya African Development (ADB) Bi. Tonia Kandiero na kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO Felchesmi Mramba.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Jakaya Kikwete, leo amezindua rasmi Mtambo wa Kufua Umeme wa Gesi Asilia wa Kinyerezi (Namba Moja).
Mtambo huo uliojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 400 na kampuni kutoka Norwey, unauwezo wa kuzalisha Megawati 150.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Rais Kikwete amesema serikali ilikuwa imeweka kipaumbele katika suala la upatikanaji umeme wa uhakika, kwa kuwa bila nishati hiyo hakuna Maendeleo ya kiuchumi.
Awali Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq, akizungumzia kuanza kazi kwa mtambo huo, amewaomba wananchi kuwa walinzi wa miundo mbinu ya umeme wa gesi asilia kwa kuwa inapita katika maeneo yao.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments System

Disqus Shortname

Comments system