KEPTENI wa Manchester United Wayne Rooney anatarajiwa kuwa fiti kwa Mechi ya Jumamosi ya Ligi Kuu England huko Goodison Park dhidi ya Klabu yake ya zamani Everton.
Rooney aliumia Enka Wiki iliyopita akiwa Mazoezini na Timu ya England ambayo yeye pia ndio Nahodha na kuzikosa Mechi zake mbili za kumalizia Kundi E la EURO 2016 dhidi ya Estonia na Lithuania.
Baada ya Mechi hiii ya Jumamosi, Man United watapaa kwenda Moscow, Urusi kucheza na CSKA Moscow katika Mechi ya Kundi B la UEFA CHAMPIONZ LIGI hapo Jumatano na kufuatia na mtanange wa Dabi ya Jiji la Manchester dhidi ya Man City Jumapili Uwanjani Old Trafford kwenye Mechi ya Ligi Kuu England
MAN UNITED – Mechi zijazo:
Jumamosi Oktoba 17
Ligi Kuu England
1700 Everton v Man United
Jumatano Oktoba 21
UEFA Championz Ligi - Kundi B
2145 CSKA v Man United
Jumapili Oktoba 25
Ligi Kuu England
1705 Man United v Man City
Jumatano Oktoba 28
Capital One Cup – Raundi ya 4
2300 Man United v Middlesbrough
Jumamosi Oktoba 31
Ligi Kuu England
1800 Crystal Palace v Man United
0 comments:
Post a Comment