Comments


HALMASHAURI NCHINI ZITENGE MAENEO YA WAZI KWA AJILI YA VIWANJA VYA MICHEZO


SAM_0096
Ofisa michezo wa wilaya ya Manyoni, Salumu Mohamedi Mkuya akiongoza ratiba ya michezo ya tamasha iliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya sekondari Kilimatinde,wilayani Manyoni.
SAM_0090
Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Manyoni, Jesca Mununo na Katibu wa CWT Wilaya ya Manyoni, Nalea Nyamuyo wakibadilishana mawazo wakati wa tamasha la michezo kwa shule za msingi na sekondari za tarafa ya Kilimatinde,wilayani Manyoni.
SAM_0086
Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Singida, Arani Jumbe ( wa nne kutoka kulia), Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Manyoni, Jesca Mununo (wa tano kutoka kulia),Ofisa michezo wa wilaya ya Manyoni, Salumu Mohamedi Mkuya (wa tano kutoka kulia), Katibu wa CWT Wilaya ya Manyoni, Nelea Nyamuyo (wa tatu kutoka kushoto) na Katibu wa CWT Mkoa wa Singida, Kitundu (wa pili kutoka kulia).
SAM_0084
Timu ya soka ya shule ya Mtakatifu Johns ya Kilimatinde wakijiandaa kucheza mchezo wao na timu ya soka ya Kilimatinde.
SAM_0074
Baadhi ya walimu wa shule ya msingi zilizokuwa zikishiriki katika tamasha la michezo wakishangaa jinsi goli lilivyoingia kwenye moja ya timu zilizokuwa zikishiriki kwenye tamasha hilo.
SAM_0076
Mwalimu Mwahija wa shule ya msingi Kilimatinde (mwenye mtandio mweupe) akipongezana na mwalimu mwenzake baada ya timu ya shule yao kupata goli la kuongoza.
   
HALMASHAURI za wilaya, Miji, Manispaa na Majiji nchini zimeshauriwa kuhakikisha zinatenga maeneo ya wazi kwa ajili ya viwanja vya michezo, ili viweze kuwasaidia watoto kufanya mazoezi na kuibua vipaji vyao mbalimbali vya michezo.

Ushauri huo umetolewa na Katibu wa CWT Wilaya ya Manyoni,Nelea Nyang’uyo kwenye tamasha la michezo lililoandaliwa na Chama Cha Walimu Tanzania Mkoa wa Singida kwa kushirikiana na Mradi wa Elimu Kupitia Michezo(ETS) kwa ajili ya kuibua vipaji vya michezo pamoja na kuwaandaa wachezaji wa siku za baadaye,lililofanyika kwenye viwanja vya shule ya sekondari Kilimatinde,wilayani Manyoni.

Huku akitoa mifano katibu huyo alifafanua kwamba baadhi ya shule zilizopo mjini Manyoni zimekuwa na maeneo finyu kutokana na kutotengewa maeneo kwa ajili ya michezo,jambo ambalo huwafanya watoto kukosa eneo la kufanyia mazoezi na hivyo kutokuwepo maandalizi ya wachezaji wa siku za baadaye.

“Pamoja na maandalizi mazuri ambayo yamefanyika lakini ni vizuri nitoe wito wakati huu kwamba michezo ilishakuwa ni burudani na inaandaa akili kwa ajili ya mwanafunzi kupokea elimu”alisema katibu huyo wa CWT wilaya ya Manyoni.
Kwa mujibu wa Nyang’uyo ni vizuri kwa Halmashauri zote nchini,hususani Halmashauri yao ya Manyoni wakahakikisha wanatenga maeneo wazi kwa ajili ya viwanja vya michezo kwa sababu maeneo yaliyo mengi yapo finyu na hata shule zingine hazijatengewa maeneo ya kutosha,hasa shsule zilizopo katikati ya mji,katika Halmashauri ya wilaya ya Manyoni hazina viwanja vya michezo.
Aidha katibu huyo alibainisha kwamba kutokana na shule hizo kutokuwa na maeneo na viwanja vya michezo jambo linalopelekea watoto kukosa eneo la kufanyia mazoezi.
“Hata wachezaji wakubwa wa kimataifa tunaowasikia leo na kuwaona wametokana na maandalizi mazuri kuanzia ngazi ya chini,kwa hiyo nitoe wito ya kwamba Halmashauri zote nchini,hususani Halmashauri ya wilaya ya Manyoni maeneo ya wazi yatengwe kwa ajili ya viwanja vya michezo ili watoto waweze kupata fursa nzuri ya kushiriki michezo”alisisitiza Nyang’uyo.
  
Kwa upande wake Ofisa michezo wa wilaya ya Manyoni,Salumu Mohamedi Mkuya alitumia fursa hiyo pia kutoa wito kwa Halmashauri ya wilaya ya Manyoni kuangalia uwezekano wa kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya michezo ili Halmashauri hiyo iweze kuendelea kufanya vizuri zaidi katika michezo mbali mbali wanayoshiriki.
“Wilaya yetu ya Manyoni imekuwa ikishika nafasi ya ubingwa wa mkoa kwenye michezo ya Umitashimta mara tatumara tatu kwenye ubingwa wa umitashimta kimkoa na kweneye mradi huu ya Elimu Kupitia Michezo (ETS) unaofadhiliwa na nchi ya Finland pamoja na CWT nao tumeshika ushindi wa kwanza mara tatu kimkoa mfululizo”alibainisha Mkuya,

Hata hivyo pamoja na kusisitiza utengwaji wa maeneo ya wazi kwa ajili ya viwanja vya michezo,lakini Mkuya hakusita pia kuwakumbusha wazazi na walezi wa wanafunzi hao kuwahamasiaha vijana wao kwa kupenda michezo,na wao wenyewe wawe mstari wa mbele kuhudhuria kwenye matamasha ya michezo ya vijana wao inapofanyika.
“Jingine naomba nitoe wito kwa Halmashauri zetu za wilaya pamoja na kutenga bajeti za michezo lakini zijitahidi kuongeza bajeti kwa ajili ya michezo ili wilaya yetu iweze kushiriki katika maeneo yote ya michezo,ikiwemo Umistashimta”alisema.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Mkoa wa Singida,Arani Jumbe alifafanua kuwa mradi huo ulioanza mwaka 2007,mpaka mwaka 2011 ulikuwa ukitoa msaada wa vifaa vya michezo kwa shule za msingi na kuanzia 2012 hadi 2014 ulikuwa kwenye shule za sekondari na hivi sasa wanatarajia kuanza kutoa vifaa hivyo kwa shule za watu binafsi.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments System

Disqus Shortname

Comments system