Comments


Algeria Kutua Nchini Kesho


Image copyrightAFP
Image captionTimu ya taifa ya Algeria
Msafara wa timu ya Taifa ya Algeria unatarajiwa kuwasili Tanzania kesho kwa ndege binafsi ya kukodi, ukiwa na jumla ya watu 65.
Msafara huo utajumuisha wachezaji 24 tayari kwa mchezo wa Jumamosi Novemba 14 dhidi ya wenyeji Tanzania katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Kocha mkuu wa timu hiyo Christian Gourcuff raia wa Ufaransa ametaja kikosi cha wachezaji 24, wakiwemo wachezaji 18 wanaocheza katika klabu za Ulaya kwa ajili ya kuikabili Tanzania.
Mchezo huu wa raundi ya pili ni wa kuwania kuingia katika hatua ya makundi ya kusaka tiketi ya kombe la dunia litakalofanyika huko nchi Urusi mwaka 2018.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments System

Disqus Shortname

Comments system