Comments


Zungu: CCM itaamua Spika wa Bunge


azani+zungu
MBUNGE mteule wa Ilala, Mussa Azzan Zungu (CCM) amesema kwa sasa hawezi kuzungumzia mbio za kuwania Spika wa Bunge hadi chama chake kitakapotoa utaratibu.
Amesema pamoja na baadhi ya makada wenzake wa CCM kuanza kujipitisha   kuwania nafasi hiyo  kwake anaamini  CCM ndicho kitatoa utaratibu wa kupatikana spika.
Zungu alitoa kauli hiyol Dar es Salaam jana alipozungumza na wanahabari baada ya jina la mwanasiasa huyo kutajwa katika  kuwania uspika wa Bunge.
Alisema yeye hajawahi kutamka kuwania nafasi hiyo zaidi ya wabaya wake wa siasa kutumia jina lake kwa malengo wanayojua wao.
“Mimi bado sijatamka kwa kinywa changu kama ninataka kuwania uspika ila utaratibu wa jambo hili utatolewa na chama.
“Hivyo  kama mnataka kujua nitawania ama laa subiri kwanza chama kitoe utaratibu ndipo nitakuwa na la kusema lakini kwa sasa hapana.
“CCM ni chama tawala kina utaratibu wake nitakuwa mtu wa ajabu kusema nitawania kuwa Spika wa Bunge wakati hata chama hakijatoa utaratibu,” alisema Zungu.
Hata hivyo, alisema  anajivunia namna bora anavyotekeleza ilani ya CCM kwa wapiga kura wake wa Ilala.
Alisema  kila mara wamekuwa msaada mkubwa kwake na wameendelea kumuamini kwa kumchagua tena.
Zungu ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Bunge katika Bunge la 10 ni miongoni mwa  wenyeviti wanaosifika kwa rekodi ya kuendesha vizuri Bunge.
Anatajwa kama kiongozi anayepewa nafasi kubwa ya kuteuliwa na chama chake cha CCM kuwania nafasi hiyo ya Spika wa Bunge ikiwa ataridhia kufanya hivyo.
Baadhi ya wabunge wa CCM na hata vyama vya upinzani wamekuwa wakimtaja mbunge huyo wa Ilala kama ni moja ya nguzo ya Bunge na hana upendeleo.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments System

Disqus Shortname

Comments system