Comments


GARY NEVILLE AFUNGASHIWA VIRAGO



BEKI wa zamani wa Manchester United na England Gary Neville ametimuliwa toka Klabu ya Spain Valencia ambako alidumu kama Kocha Mkuu kwa muda usiozidi Miezi Minne.
Neville, mwenye Miaka 41 na ambae pia ni Msaidizi wa Meneja wa Timu ya Taifa ya England Roy Hodgson, aliteuliwa kuiongoza Valencia Mwezi Desemba.
Tangu wakati huo, Valencia ilishinda Mechi 3 tu kati ya 16 za La Liga na Mechi 10 kati ya 28 walizocheza chini ya Neville.
Huku akikiri kuwa alitaka abaki Valencia na pia kuungama kuwa matokeo hayakuwa ya kiwango chake au Klabu, Neville amekubali amepaswa kuwajibika.
Balaa na kusakamwa kwa Neville kutakiwa kung’oka na Mashabiki wa Valencia kulianza Mwezi Februari waliponyukwa Bao 7-0 na Barcelona kwenye Mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya Copa del Rey.
Mbali ya kutamkwa kutimuliwa kwa Gary Neville lakini hatima ya Mdogo wake Phil Neville ambae ni mmoja wa Makocha wa Valencia na alikuwa hapo hata kabla Gary kutua huko bado hakujawekwa bayana.


Kwa sasa Valencia itakuwa chini ya Meneja Msaidizi wa zamani wa Liverpool Pako Ayestaran, mwenye Miaka 53, hadi mwishoni mwa Msimu.
Image result for PAKO AYESTARAN
Kocha mpya wa valencia Pako Ayestaran

Kwenye La Liga, Valencia wapo Nafasi ya 14 wakiwa Pointi 6 tu juu ya zile Timu za kushushwa Daraja huku Gemu zikibaki 8 hadi Msimu kwisha.
LA LIGA
Jumapili Machi 20
Ratiba
Ijumaa Aprili 1
2130 Rayo Vallecano v Getafe CF
Jumamosi Aprili 2
1700 Atletico de Madrid v Real Betis
1915 Las Palmas v   Valencia C.F
2130 FC Barcelona v Real Madrid CF
2305 Celta de Vigo v Deportivo La Coruna
Jumapili Aprili 3
1200 Athletic de Bilbao v Granada CF
1600 Malaga CF v RCD Espanyol
1815 SD Eibar v Villarreal CF
2030 Sevilla FC v Real Sociedad
Jumatatu Aprili 4
2030 Levante v Sporting Gijon
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments System

Disqus Shortname

Comments system